Serikali ina matarajio makubwa ya utekelezaji wa Miradi ya Kilimo cha Umwagiliaji kutokana na ongezeko kubwa la Bajeti ya fedha za miradi ya Maendeleo kwa Mwaka wa fedha 2022 – 2023, hatua hii ya Serikali ina lenga kuongeza uzalishaji wa Mazao ya chakula na Biashara kutokana na kilimo cha Umwagiliaji.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Reymond Mndolwa alipokuwa akizungumza na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Makao Makuu jijini Dodoma.
Kufuatia hatua hiyo ya Serikali kuongeza kiasi hicho cha fedha Shillingi Bilioni 146.5 Katika Sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji Bw. Mndolwa ametumia fursa hiyo kuwaasa watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kupendana kushirikiana, kufanyakazi kwa pamoja (time work) kwa kuzingatia weledi katika maeneo yao ya kazi.
Amesisitiza kuwa suala la kupendana na kuheshimiana katika Utumishi linaongeza ufanisi katika utendaji kazi na kuleta amani.
“Tuheshimu kila mmoja aliyepo hapa, wote thamani yetu ni moja kwa sababu wote tunaitumikia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.” Alisisitiza
Bw. Mndolwa ameongeza kwa kusema kuwa watumishi wanao wajibu wa kuhakikisha wanatunza mali zote za Tume akitolea mfano magari na Mitambo inayotumika katika shughuli za ujenzi wa miradi ya Umwagiliaji.
“Nataka kila mtu ahakikishe anatunza mali ile aliyokuwa nayo” ili iweze kutusaidia kwa muda mrefu zaidi, itunze ione ni mali yako wewe, usione ni mali ya umma au serikali, sababu serikali ni mimi na wewe “kwahiyo naomba wale wanaoendesha vyombo vya Mamlaka na wale wanaovipanda wavitunze.”
Kikao hicho cha Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ni cha kwanza mara baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan mapema Mwezi huu.

Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya
Umwagiliaji Bw, Reymond
Mndolwa akifafanua jambo mbele ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji alipokuwa akizungumza nao Makao Makuu jijini Dodoma
Baadhi ya
Watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakimsikiliza Mkurugenzi
wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw, Reymond Mndolwa (Hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na watumishi wa Tume hiyo Makao Makuu jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...