Saa chache kabla ya kuzinduliwa rasmi filamu ya Royal Tour ya Tanzania tayari mwanga na manufaa yake yameanza kuonekana ambapo wafanyabiashara na watu wengine mashuhuri walioona vipande vya awali vya filamu hiyo na kuvutiwa leo wamekutana na Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye klabu ya faragha ya Lotos hapa New York, miongoni mwa waliohudhuria ni Meya mashuhuri wa jiji la New York, Eric Adams, ambaye ameeleza kuipenda Tanzania na kuahidi kuitangaza zaidi katika jiji lake la New York.

Mtu mwingine mashuhuri aliyehudhuria ukiondoa mabilionea na wamiliki wa makampuni makubwa duniani ikiwemo watangazaji wa CNN, CBS nk alikuwa ni Gayle King mtangazaji mashuhuri wa vipindi vya CBC Mornings na “King in the House”

Gayle kwa hapa Marekani ni mtu mashuhuri akijulikana pia kwa urafiki wake wa karibu na wa miaka mingi na nguli mwingine Oprah ambako pia yeye Gayle ni Mhariri wa jarida la Oprah la O Magazine!

Jioni hii na usiku wa manane kwa saa za Tanzania, Rais Samia ataizindua filamu hiyo katika ukumbi wa Guggenheim Museum New York.Source: Diaspora News!



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...