Na Humphrey Shao,Michuzi Tv

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022, Sahili Geraruma ameonesha  kusikitishwa na hali ya udanganyifu  wa nyaraka na dharau  katika  ujenzi wa Zahanati ya Kawe  wilayani Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam , hivyo kuamua kutoweka  jiwe la msingi katika mradi huo.

Akizungumza mara baada ya kupitia nyaraka za Manunuzi kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge  wa Uhuru 2022 ametoa tuhuma hizo na kisha kuwaba  radhi wakazi wa Kawe baada ya  kuchelewa kutoka ndani kwasababu ya ugumu wa nyaraka zilizowassilishwa katika eneo hilo.

Akielezea zaidi amesema “Kwanza viongozi  wa manunuzi  wa eneo hilo wameonyesha dharau kubwa kwani  licha ya kutangaza jukwaani Kuwa wakifika kwenye mradi wakute  nyaraka lakini bado wameonesha ukaidi.”

Ameongeza  pili kumekuwa na udanganyifu katika Manunuzi ya Vigae (Tiles) ambazo zilitakiwa kuwekwa na kuwekwa saizi nyingine.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge kitaifa amesema kwa  upande wa Manunuzi umefanya udanganyifu wa nyaraka za ununuzi wa nondo ambazo certificate zake ni za mradi wa madarasa ya Uviko 19 wakati kinachojengwa ni Zahanati.

Kutokana na tuhuma hizo za ufanganyifu wa nyaraka ameamua kutoweka jiwe la msingi katika Zahanati hiyo na kuagiza  Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) kufanya  ukaguzi ndani ya siku tatu.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Godwin Gondwe akipokea Mwenge kutoka kwa Katibu tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam , Hassan Abbas Lugwa  katika Viwanja vya Bunju A Kinondoni.



Viongozi wa Manispaa ya Kinondoni wakiwa katika picha ya Pamoja mbele ya Mwenge wa Uhuru na kiongozi wa Mbio za Mwenge, Sahil Geraruma.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni,Khanifa Suleiman Hamza akitoa maelezo Kwa mmoja wa wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2022
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wakipitia nyaraka za mradi neno Kwa neno wakati wa kukimbizwa Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Kinondoni.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Godwin Gondwe akikabidhi Lisala ya Utii Kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Sahil  Geraruma mara baada ya kukagua miradi yote

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...