i. Kuimarisha utoaji wa huduma za chanjo kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano;
ii. Kusimamia viwango vya ubora wa huduma za kinga na tiba katika ngazi zote za utoaji huduma za afya nchini;
iii. Kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, vifo vya watoto wachanga pamoja na mimba za utotoni,
iv. Kuimarisha upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya
v. Kuimarisha huduma za lishe hususani kwa watoto wa umri wa chini ya miaka 5, vijana balehe na wanawake wa umri wa kuzaa;
vi. Kuimarisha huduma za afya na usafi wa mazingira ili kudhibiti magonjwa ya kuambukizi na hivyo kupunguza idadi ya wagonjwa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini;19

vii. Kuimarisha miundombinu ya kutolea huduma za afya ikiwemo katika Hospitali za Rufaa za Mikoa, Kanda, Maalum na Taifa;
viii. Kuimarisha huduma za matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi;
ix. Kudhibiti magonjwa ya mlipuko, magonjwa ya kuambukiza na magonjwa yasiyo ya kuambukiza;
x. Kuimarisha utoaji wa mafunzo ya wataalamu katika Sekta ya Afya;
xi. Kuimarisha mifumo ya ugharamiaji wa huduma za afya nchini;
xii. Kuimarisha utawala bora na uwajibikaji katika utoaji huduma za afya; na
xiii. Kuimarisha mifumo ya TEHAMA na matumizi ya takwimu katika utoaji wa huduma za afya nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...