Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa Hati ya Ushirikano (MoU) mbili Ikulu Entebbe nchini Uganda.

Hati hizo ni pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa 400KV kutoka Masaka-Mutukula-Nyakanazi -Mwanza na nyingine ni kuhusu ushirikiano wa masuala ya Ulinzi na Usalama baina ya nchi hizo mbili.

Aidha, utiaji saini huo ulishuhudiwa pia na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ambapo amesisitiza kuendelea kushirikiana kwenye utenngenezaji wa chanjo na dawa za binadamu na mifugo.

Makubaliano pia ni kwamba Tanzania itaanza kununua dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI (ARVs) kutoka Uganda.

Miongoni mwa mengine yaliojadiliwa ni kufunguliwa upya kwa njia ya Mwanza - Port Bell Kampala, ambayo hapo awali ilikuwa haifanyi kazi lakini hivi sasa inafanya kazi.

Kwa sasa njia hiyo imepunguza kwa kiwango kikubwa muda wake wa mpito ambapo sasa huchukua siku 4 tu tofauti na siku 9 hapo awali, hivyo kupunguza gharama za kufanya biashara.

Wakati huo huo, Tanzania imekubali kupunguza gharama za usafirishaji ambapo kwa sasa Uganda italipa Dola za Kimarekani 10 kwa lori litakalopita kila kilomita 100 katika njia ya kutoka Mutukula hadi Dar es Salaam kuanzia mwaka mpya wa fedha Julai mosi mwaka huu.

Pia, Uganda imeahidi kutuma tani nyingine elfu 10 za sukari ili kufidia upungufu wa bidhaa hiyo Tanzania.


ZuhuraYunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...