Balozi wa Canada nchini Mh. Pamela O'Donnell (wa pili kutoka kushoto) akigonga glasi na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Barrick wakati wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Canada iliyofanyika nyumbani kwa balozi jijini Dar es Salaam. Barrick ni mmoja wa wadau waliofanikisha hafla hiyo.
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahi pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wanawake na Makundi maalum,Dk.Doroth Gwajima (aliyevaa kofia) wakati wa hafla hiyo.
KAMPUNI ya Barrick nchini Tanzania imekuwa mmoja wa wadau wakuu waliofanikisha maadhimisho ya Siku ya Canada, ambapo baadhi ya wafanyakazi wake walishiriki katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Canada nchini Masaki jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Barrick waliohudhuria katika hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Canada nchini,Mh. Pamela O'Donnell.
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahi na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...