Waziri wa Nishati January Makamba amesema uendeshaji umahiri na umadhubuti wa uongozi wa shirika la TPDC, ni Jambo ambalo serikali unalipa uzito wa hali ya juu.

Makamba Ameyasema hayo wakati akizindua bodi ya wakarugenzi wa shirika hilo jijini Arusha na kueleza kwamba uteuzi wa bodi hiyo unaakisi dira na Malengo mapya ya serikali kwa shirika hilo kuelekea katika mafuta na gezi.

Amesema bodi hiyo chini ya mwenyekiti wake balozi Ombeni Sefue inakidhi nafasi ya TPDC katika maendeleo ya nchi, Dira na mwelekeo mpya wa TPDC katika uchumi mpya wa Gesi na maendeleo ya mafuta nchini kwa ujumla.

"Dhamira yetu ni kuona shirika hili linatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi na sio katika mapato tu bali uendeshaji wa rasilimali watu katika tasnia hii lakini pia ushiriki wa nchi katika miradi mikubwa ya kimkakati ya mafuta na Gesi" Alisema Makamba

Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi hiyo ya TPDC Balozi Ombeni Sefue ambaye pia ni katibu mkuu Kiongozi mstaafu amesema wao kama bodi kazi yao ni kwenda kuchangamsha na kuhakikisha kila kitu kinaenda inavyotakiwa na sekta hii ili taifa liweze kunufaika na rasilimali zake za mafuta na Gesi tulizopewa na Mungu.

Mikakati iliyopo kwa sasa ni ile ya serikali na haijaanza leo tutaipitia kama bodi mpya tumefanikiwa wapi na changamoto ni zipi na zitatatuliwaje ili kazi iendelee vizuri kujenga TPDC yenye kusaidia serikali.

Awali Mkurugenzi wa Shirika la mafuta na Gesi nchi muhandisi James Maragio amesema kuwa miradi ya mafuta na Gesi itakapokamilika itasaidia kutatua changamoto za wananchi.

Alisema kuwa wana miradi mikubwa ikiwemo mradi wa bilion 40 ikiwemo mradi wa kujenga bomba la mafuta kutoka hoima Uganda ambao umeonyesha mafanikio pia kuna maradi wa kutafuta mafuta katika bonde la ufa ambao upo kwenye Mchakato.

Picha wajumbe wa bodi ya TPDC wakiwa katika picha ya pamoja na waziri wa nishati January Makamba Leo mara baada ya kuzindua bodi hiyo.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...