Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Modestus Lumato (kulia aliyesimama) akizungumza katika kikao kazi na Wahariri wa vyombo vya habari kilichofanyika leo Julai 16,2022 Jijini Dar es Salaam kilicholenga kufahamiana na kubadilishana mawazo kwa pamoja ambapo pia Mkurugenz huyo amezungumzia matumizi ya Gesi kwenye magari na majumbani na kupanda kwa Bei ya mafuta. (kushoto aliyekaa) ni Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) Deodatus balile.
 
 Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) Deodatus balile (kushoto aliyekaa) akipiga makofi kupongeza hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Modestus (kulia anaezungumza) wakati alipokuwa akizungumza katika Kikaokazi hicho.


MKURUGENZI Mkuu wa Ewura, Mhandisi Modestus Lumato amekutana na kufanya kikao kazi na wahariri wa vyombo mbali mbali kutoka Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) kujadiliana juu ya matumizi mbadala ya gesi kwenye magari na hata majumbani hususani Vijijini ambako wamekuwa wakitumia zaidi kuni na mkaaa.

Katika majadiliano hayo yaliyofanyika leo Julai 16, 2022 katika ukumbi wa Kisenga millennium Tower eneo la Kijitonyama Dar es Salaam pamoja na mambo mengine, Lumato amepokea ushauri mbalimbali kutoka kwa wahariri hao na kujibu maswali huku pia wamejadili kupanda kwa bei za mafuta.

Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) Deodatus balile  (kushoto aliyesimama) akizungumza kwenye mkutano huo.
Afisa Mwandamizi Huduma kwa wateja wa EWURA Kanda ya Mashariki Getrude Mbiling'i akifuatilia mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...