Na.Khadija Seif, Michuzi Tv


NAIBU Waziri Utamaduni, Sanaa na Michezo, Pauline Gekul amezindua rasmi Kamati maalum ya kushughulikia malalamiko ya wasanii na wadau mbalimbali wa sanaa kuhusu mgao wa Mirabaha kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Taasisi ya Hakimiliki nchini.

Akizungumza katika uzinduzi huo kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa, Naibu Waziri Pauline Gekul amesema serikali imejipanga vyema katika kushughulikia chagamoto za malalamiko ya wasanii kwa Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (Cosota), kwa kuunda kamati hiyo yenye mkusanyiko wa wadau muhimu.

Naibu Waziri Gekul amesema Waziri Mchengerwa anategemea kamati hiyo itapendekeza mifumo bora zaidi ya kukusanya na kugawa mirabaha inayoshabihiana na mifumo inayotumika kwengineko duniani, kupendekeza njia bora zaidi ya kupambaa na uharamia wa kazi za wasanii pamoja na kupendekeza mifumo bora zaidi ya utendaji wa Taasisi ya Hakimiliki.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kuratibu namna bora ya kusimamia Hakimiliki nchini, Victor Tesha amesema wataweka nguvu yao yote usiku na mchana kadri wawezavyo kusapoti nguvu kubwa katika kuboresha ufanisi.

"Naomba kutoa ahadi kwamba mimi na wenzangu wote tulioteuliwa tutafanya kazi kwa weledi na ubunifu mkubwa ili kuhakikisha namna bora ya uratibu wa hakimiliki na maslahi ya serikali na wasanii yanatimia, tutahakikisa tunapokea maoni ya kila mdau na kufanya vikao na wote na kuishauri serikali kwa kadri inavyowezekana."


Naibu Waziri Pauline Gekul akizungumza na kamati maalum Jijini Dar es salaam, iliyozinduliwa rasmi Kwa ajili ya kushughulikia Malalamiko ya Mirabaha Kwa Wasanii nchini


Mwenyekiti wa Kamati ya Kuratibu namna bora ya kusimamia Hakimiliki nchini Victor Tesha akizungumza na waandishi wahabari mara baada ya kuzinduliwa kwa Kamati hiyo iliyopewa majukumu ya kuhakikisha inafanya utafiti wa namna gani wasanii watalipwa Mirabaha yao bila upendeleo pamoja na kukusanya Malalamiko yao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...