NA BALTAZAR MASHAKA, Ilemela

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  Sahili Geraruma amezindua mradi wa maji wa Mlimawa rada wilayani Ilemela uliojengwa kwa zaidi ya sh.milioni 365.5 nakuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.

Akizundua mradi huo uliojengwa na mkandarasi mzawa kampuni ya kizalendoya URSINO LTD, Geraruma alisema umetekelezwa kwa ubora wa viwango kulingana na thamani ya fedha za walipa kodi na kuipongeza kwa kazi hiyo nzuri.

 
“Nimeridhishwa na mradi huu kwa namna ulivyotekelezwa na kampuni ya kizalendo ikiongozwa na wazawa, imeufanya kwa weledi, umetoa ajira kwa wananchi na wamepata kipato, umekamilika na  utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi waKiseke na maeneo jirani,”alisema.


Awali Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa MazingiraJijijni Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Leonard Msenyele,alisema mradi huo  umetekelezwa kutokana na mahitaji ya huduma ya maji kwa wananchi na sera ya maji ya mwaka 2002,Mpango Mkakati wa Maji nautekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020-2025.


Alisema mradi huo umegharimu sh.365,580,080 kwa fedha za serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko -19, umekamilika kwaasilimia 100 utaanufaisha wakazi 3,600 wa Kiseke, katika Manispaa ya Ilemela.


“Mradi huu utasaidia upatinakaji wa huduma ya  maji katika Kata ya Kiseke, hasa wakazi nawananchi wanaoishi katika miinuko (mlima wa Rada),utwanufisha wananchi 3,600 nautaongeza kiwango cha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.


Mkurugenzi wa Kampuni ya URSINO Ltd, Mhandisi Mnandi Mnandialisema kazi iliyotekelezwa katika mradi huo ni kulaza bomba kuu lakusafirishia maji la urefu wa km 3,kulaza mabomba ya kuzambazia maji, ujenzi wachemba tatu,usimakaji wa pampu yenye uwezo wa kuzalisha lita 35,000 za  maji kwa saa na ujenzi wa tenki la kuhifadhiamaji  lenye ujazo wa lita 150,000. 


“Niishukuru serikali ya awamu ya sita  kwa kutupatia kazi ya kujenga miundombinu yamaji kwa manufaa ya wananchi wa Kiseke na kuhakikisha inakamilika na kupatahuduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao,”alisema Mhandisi Mnandi na kuahidi kuendelea kufanya kazi mbalimbali za miradi ya huduma ya jamii kwa weledi endapo watapewa kazi na serikali.


Aidha Mary Protas,mkazi wa Kiseke, alisema kukamilika kwa mradihuo wa maji ni faraja kubwa kwa wananchi wa eneo hilo, kwa sababu walikuwa wakipata adha kubwa yahuduma ya maji safi na salama kwa wa matumizi mbalimbali, pia walilazimika kuamka usiku kupanga foleni ili kupata maji.

“Kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Kiseke na mlima wa rada hasa  wanawake tunamshukuru sana Rais Samia SuluhuHassan kwa kusikia kilio chetu na kutujali kasha akatoa fedha za kujenga mradihuu, tunaahidi kuwsimama naye muda wote,”alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...