Na Janeth Raphael  - Dodoma

SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana na  Brazil zimesaini mkataba wa mradi wa utafiti wa mbegu ya pamba,usalama wa chakula na masuala ya lishee wenye thamani  jumla ya Dola za Marekani 930,118  kwa lengo la kuimarisa utafiti pamoja na kuongeza Thamani ya zao la pamba hapa nchini.

Wakisaini mkataba huo leo jijini Dodoma akiwepo Balozi wa Brazili Nchini Tanzania,Antonio Cesar,Mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP),Gunga Mbavu ambaye alimwakilisha mgeni rasmi katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo na Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania,Marco Mtunga.

Mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP),Gunga Mbavu ambaye alimwakilisha mgeni rasmi katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo Amesema mradi huo wa BEYOND COTTON PROJECT utanufaisha kaya Zaidi ya kaya 8800  kwa dhumuni la kuimarisha tija katika uzalishaji wa zao la pamba.

“Matarajio yetu wakulima kaya kama 8800  watanufaika katika mradi huu zikiwemo asilimia 50 ya vijana watanufaika na mradi huu utatekelezwa katika mkoa wa mwanza,tumepanga ifikapo mwaka 2030 kilimo kikue kwa asilimia 10,na mradi huu umelenga agenda za kilimo tulizo jiwekea’’ Amesema

Balozi wa Brazili Nchini Tanzania,Antonio Cesan amesema kuwa Brazil wataendelea kushirikiana na nchi ya Tanzania kwa kuimarisha kilimo cha Pamba ili kuwa na tija katika zao hilo.

Naye Mkurugenzi mkuu  wa Bodi ya Pamba Tanzania,Marco Mtunga ameeleza kuwa pamba ni zao ambalo litaongeza tija kwa mkulima pamoja na  vijana kuweza kujikwamua kimaisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mbegu TARI,Dr Geofrey Mkamilo amesema kuwa Taasisi hiyo itaendelea kufanya utafiti wa mbegu bora ambazo zitaongeza tija kwa wakulima wapamba Pamoja na kuleta matokeo chanya kwa wakulima.

Mradi huo wa   kilimo cha pamba utatekelezwa katika mkoa wa Mwanza pamoja na wilaya zake ikiwemo Wilaya ya Magu,Misungwi  na kwimba.

Balozi wa Brazil nchii Tanzania Antonio Cesan akizungumza Wakati wa mkutano huo
Mkurugenzi wa Shirika la chakula Duniani (WFP) Gunga Mbavu akizungumza katika mkutano huo wa kusaini mkataba
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya pamba Marco Mtunga akizungumza mara Baada ya kusaini mkataba huo
Mkurugenzi Mkuu Tari Dkt Geoffrey Mkamilo akizungumza katika mkutano huo wa kusaini mkataba



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...