Kiongozi mashuhuri duniani wa kiroho na Balozi wa Amani, Gurudev Sri Sri Ravishankar ameondoka nchini leo asubuhi kuelekea Ujerumani baada ya kukamilisha “Royal Tour” ya siku mbili nchini.

Akiwa hapa nchini,pamoja na mambo mengine, alihudhuria Tamasha la Utamaduni la Tanzania na India, kuendesha mazoezi ya kutumia njia za kupumua, kuhutubia mkutano wa Biashara kati ya Tanzania na India na kutembelea Zanzibar ambako pia alikutana na Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi.

Akiagana kwenye hotel ya Hyatt na baadaye Uwanja wa Ndege na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi, Bw. Gurudev ameahidi kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika sekta za utamaduni na michezo ikiwemo kuahidi kualika vikundi vya sanaa na utamaduni kuhudhuria Tamasha lake kubwa liitwalo “World Cultural Festival” ambalo mwaka jana lilihudhuriwa na wasanii 37,000 kutoka nchi 155 duniani na likikusanya takribani watu milioni 3.7 pamoja.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...