Na Mwandishi wetu, Mirerani
Mwenyekiti
 wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Kiria Laizer ameongoza 
harambee ndogo ya kumchangia mtoto yatima ambaye ni mwanafunzi wa chuo 
cha utumishi wa umma Tanga anayesomea diploma ya utunzaji kumbukumbu ya 
nyaraka.
Kiria, ameongoza
 shughuli ya kumchangia msichana huyo Maureen Laizer ambaye anaishi na 
mama yake kwenye kata ya Endiamtu na kufanikisha kupata shilingi 
500,000.
Awali, harambee 
hiyo ngodo ilifanyika na kupatikana shilingi 200,000 ila Kiria 
akaongezea shilingi 300,000 na kupatikana shilingi 500,000 
zitakazotumika kwenye masomo ya mwanafunzi huyo.
Kiria
 akizungumza kwenye shughuli hiyo ya harambee amesema kuchangia elimu ni
 jambo jema kwenye jamii kwani hivi sasa msingi mzuri wa watoto ni 
kupatiwa elimu.
“Mtoto 
huyu amejitahidi hadi kufikia hatua hii ya kuwa mwanafunzi wa chuo hivyo
 ni vyema akasaidiwa ili aweze kuhitimu masomo yake anayosomea mkoani 
Tanga,” amesema Kiria.
Mwenyekiti
 wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Mirerani Adam Kobelo amewapongeza viongozi 
na wananchi waliochanga na pia Kiria kwa kufanikisha harambee hiyo ndogo
 kwa kutoa fedha zake binafsi shilingi 300,000.
Hata
 hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Dk Suleiman Serera amemtaka 
mwanafunzi huyo kuhakikisha anasoma kwa bidii ili aweze kutimiza ndoto 
zake na pia kutumikia Taifa hapo baadaye.
“Pia
 unapaswa kutambua kuwa hakuna haki isiyokuwa na wajibu, unachangiwa 
fedha za masomo lakini ofisa mtendaji wa kata atafuatilia huko chuoni 
kwenu ili kuangalia maendeleo yako,” amesema Dk Serera.
Kwa
 upande wake mwanafunzi huyo Maureen amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya, 
Mwenyekiti wa CCM na viongozi wote waliofanikisha yeye kuchangiwa na 
kupata fedha hizo za ada za masomo.
“Nawashukuru
 wote waliofanikisha mimi kupata msaada huu wa ada ya masomo na 
ninawaahidi kusoma kwa bidii kwenye masomo yangu huko chuoni Tanga,” 
amesema.
Mwenyekiti
 wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Kiria Laizer (kushoto) 
akimkabidhi shilingi 5,000 mwanafunzi wa stashahada ya utunzaji 
kumbukumbu ya nyaraka katika chuo cha utumishi wa umma Tanga, Maureen 
Laizer kwa ajili ya ada ya masomo yake.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...