Na.Khadija Seif,Michuzi TV 


KLABU ya Gofu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ)Lugalo inatarajiwa kusafiri hii leo kwenda Malawi kwaajili ya shindano la siku Nne Kuwaenzi mashujaa wa Vita ya Pili ya Dunia.

Mkurugenzi wa Michezo na Utamaduni JWTZ  Kanali Martin Msumari amesema,timu ipo katika maandalizi ya mwisho na wachezaji 12 watakwenda kushiriki shindano hilo.

Naye Brigedia Jenerali Joseph Mbilinyi amesema,mpaka sasa timu yao ipovizuri kwaajili ya shindano na wanatumai wataweza kufanya vizuri kama shindano walivyofanya katika shindano la Mkuu wa Majeshi “NMB CDF TROPHY”lilofanyika nchini mwezi uliopita. 

Balozi Mstaafu Job Masima amesema,wao kama wachezaji wamejipanga kikamilifu kwaajili ya shindano hilo na wanatarajia kwenda kufanya vizuri na kurudi na ushindi nyumbani.

Wachezaji 12 Wakiongozwa na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara na Meja Jenerali Ibrahim Mhona na Mwenyekiti wa Lugalo Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo ni miongoni mwa Wachezaji hao.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...