WAANDISHI wa habari wameomba kushirikishwa kila hatua yanayofanyika katika Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ili kupata uwanda mpana wakuwajuza wananchi kuhusu mambo mbalimbali katika Jumuiya hiyo.

Wito huo umetolewa na wandishi wa habari wa vyombo tofauti waliposhiriki semina ya kuwajengea uwezo kuhusu Jumuiya hiyo iliyoandaliwa na Mtandao wa wakulima  wa Afrika Mashariki na nchi za Kusini mwa Afrika (ESAFF)  kwa kushirikiana na Kituo cha Malengo ya Maendeleo Endelevu Afrika (SDGCA).

Semina hizo ni moja ya utekelezaji wa Mradi wa Mpango Jumuishi wa Kujenga Uwezo wa Kitaasisi (IICB) kwa Sekretarieti ya SADC na Wadau wa Kitaifa kwa kushirikiana na wadau wake katika kufikia ahadi za kikanda hususan, Mpango Elekezi wa Kikanda wa Maendeleo (RISDP) - (2020-2030) na Dira ya 2050 ya SADC. 

Kati ya waliotoa maoni namtazamo juu ya Jumuiya hiyo ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN) Salome Kitomari ambapo alisema katika kuhabarisha huko kwa sasa kinachofanywa ni waandishi kutakiwa wakati kunapokuwa na matukio kama vile ujio wa viongozi na mikutano mbalimbali mikubwa inayofanyika.

Amesema hii ni tofauti na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao wamekuwa wepesi katika kutoa taarifa na kufungua milango ya kupata taarifa muda wowowte wanapohitajika.

“Kutokana na hilo waaandishi wanajikuta wanafunga kwa kuripoti tukio la mkutano ,au kusubiri taarifa kutoka wizarani au Ikulu kuhusu yanayojiri katika Jumuiya hiyo jambo ambalo halina afya katika taaluma ya habari licha ya kuwa kuna mambo mengi yakuandika kuhusu Jumuiya hiyo kikiwemo changamoto, mafanikio na fursa mbalimbali zilizopo kwa nchi wanachama.

Kwa upande wake Tausi Mbowe kutoka kituo cha redio Times, amesema kumekuwepo na utoaji wa tuzo za waandishi wanaoandika habari za SADC, lakini ni kama kwa upande wa Tanzanaia zinawabagua kwa kuwa wengine huandika kwa lugha ya Kiswahili.

Amesema ifike mahali kwa kuwa Kiswahili kimechaguliwa kuwa lughha ya kuzungumzwa na umoja huo,basi katika shughuli zake zote lugha hii ipewe kipaumbe.

“Tunaandika sana Makala zinzohusu SADC, lakini zikifika kwa majaji inaelezwa zimeandikwa kwa lugha ya Kiswahili, hii sio sawa na kama ni katika kuwaridhisha wafadhili wa tuzo hizo basi vema kukawe kwa majaji wanaojua lugha hii ili iwe rahisi kuzipitia zinazotoka Tanzania,”,alisema  Tausi.

Aidha kwa upande wake Dorcus Raymond kutoka Channel Ten, alisema bado kuna ukitirimba katika kupata taarifa kwa wadau mbalimbali waandishi wanapotaka kukamilisha habari zao.
Zaah alipendekeza kuwepo kwa klabu  za SADC  kuanzia shule nakwenye mashirikisho ya sekta mbalimbali yatayakosaidia kushua elimu na taarifa ya Jumuia hiyo.

 Philipo Mhava kutoka redio Clouds,amesema hata lugha ya Kiswahili imekuwa ngumu kutumika katika utoaji taarifa unazohusu Jumuiya hiyo na kuwatenga hata watanzania wakawaida kuifahamu na kufuatilia yanayoendelea ndani ya Jumuiya hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa ESAFF, Joe Mzinga,amesema malengo ni kuhakikisha vyombo vya habari vinajengewa uwezo na kuwezeshwa kuweza kutoa habari zaidi kuhusu SADC, aliongeza kua kuna haja ya kushirikisha vyombo vya habari katika ngazi zote, tafsiri ya taarifa mbalimbali ili kuakisi muktadha wa ndani, kutoa mafunzo kwa vyombo vya habari kuhusu jinsi ya kusambaza taarifa, kuandaa utaratibu wa ushiriki wa kimkakati wa AZAKi-Vyombo vya Habari, makala ya video ya baadhi ya mafanikio kuhusu ushirikiano wa kikanda wa SADC.

Mzinga ameeleza kuna makundi mbalimbali yanapaswa kushirikishwa katika Jumuiya hiyo ikiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, madhebu ya dini na taasisi zingine na hakuna anayepaswa kuchwa nyuma.

Akizungumza kwenye washa hiyo, Ambrose Rwaheru kutoka SDGC amesema shirika lake litaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu mtangamano wa SADC.

Mradi huo umefadhiliwa na Umoja wa Ulaya na unatekelezwa katika nchi za Tanzania, Malawi, Zambia na Zimbabwe,
Mwandishi wahabari Dorcus Raymond kutoka Channel Ten, alisema bado kuna ukitirimba katika kupata taarifa kwa wadau mbalimbali waandishi wanapotaka kukamilisha habari zao
Ambrose Rwaheru kutoka SDGC amesema shirika  shirika lake litaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu mtangamano wa SADC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...