Msaani wa Bongo Fleva Diamond Platinum pamoja na mchekeshaji maarufu kwa jina la Joti ambao ni mabalozi wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania, jana walijiunga na wafanya kazi wa kampuni ya Airtel kwenye sherehe za kuanga mwaka ambazo zilifanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya wafanya kazi wake.

Kwenye sherehe hizo, wasanii Hao walitoa burudani ya kutosha na kuwapagawisha wafanyakazi hao wa Airtel.

Akizungumza mara baada ya sherehe hizo, msanii Diamond aliwashukuru uongozi wa Airtel kwa kumpa heshima ya kualikwa na kuwa pamoja kwenye sherehe hizo za kufunga mwaka.

'Ninayo furaha na heshima kwa uongozi wa Airtel kwa kunichangua kuwa balozi wa kampuni yao, lakini pia nawashukuru sana kwa kunialika na kuwa na nyinyi hapa kwa siku Leo. Tupo wasanii wengi lakini mkaona ya kwamba nafaa kushiriki nanyi, nawashukuru sana' alisema Diamond.

'Nimekuwa balozi kwa huduma na bidhaa za kampuni ya Airtel. Naomba kuwahidi kuwa nitaendelea kuwa mfano ili kuendelea kuiweka Airtel kuwa kampuni namba moja hapa nchini kwa huduma za simu za mkononi' aliongeza Diamond.

Akizungumza kwa niaba ya wafanya kazi wa Airtel, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Bw, Dinesh Balsighn  alisema kuwa Airtel inathamini sana mchango wa wafanya kazi wake na ndio maana imeandaa sherehe hizi ill kuwakutanisha pamoja na kusherekea mafanikio ya mwaka 2022.

'Bila wafanya kazi hawa tusingekuwa tunafurahia mafanikio ya mwaka 2022. Juhudi zetu ndio zimefanya Airtel kuwa hapa ilipo. Tutaendelea kudhamini juhudi hizi ili kuendelea kukua kwa pamoja' Balsingh alisema.

'Nachukua fursa hii pia kuwashukuru mabalozi wetu Diamond na Joti kwa kukubali mwaliko wetu na kuja kujumuika nasi hapa Leo. Tumefurahi pamoja na kwa kweli tumeona mafanikio Kupitia kwenu na tutaendelea kufanya kazi pamoja kwa siku za mbeleni, aliongeza Singano.

























Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...