Na Abel Paul wa Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi la Mkoa wa Arusha limetoa huduma ya matibabu na ushauri wa kiafya katika kituo cha AST maalumu kwa ajili ya kuwalea wazee wanaoishi katika mazingira magumu Jijini Arusha.

Mwenyekiti wa mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Arusha (TPF NET) Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP MARY KIPESHA amebainisha kuwa kupitia mtandao huo wametoa msaada wa vitu mbalimbali pamoja na huduma ya kiafya ikiwa mwendelezo wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoani humo.

ACP Kipesha amesema mbali na kutoa msaada huo, katika siku hizo 16 za kupinga ukatili amebainisha kuwa wametoa elimu katika shule, hospitali, nyumba za ibada, masoko pamoja na stendi za mabasi ambapo jamii imepata uelewa wa kutosha.

Mkurugenzi wa Kituo hicho Bi. Ester Njau amelishukuru Jeshi hilo kwa kutoa matibabu kwa wazee wanaoishi katika kituo hicho ambapo amebainisha kuwa matibabu hayo pamoja na vitu mbalimbali vilivyotolewa vitaboresha afya za wazee hao.

Naye Bi. Mary Wakati akisoma risala amesema kuwa awali walifanya uchunguzi na kubaini kuwa wazee wengi maeneo mbalimbali katika mkoa wa Arusha wanakabiliwa na mazingira magumu ya kuishi pamoja na jamii kushindwa kutambua uwepo wa wazee na kushindwa kuwahudumia.

Aidha Bi. Regina Eusebi kwa niaba ya wazee wenzake mbali na kushukuru Jeshi la Polisi kwa msaada walioutoa ametoa wito kwa makundi mengine kutoa misaada katika vituo vinavyolea watu wenye uhitaji mbalimbali.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Elerai Bwana Losioki laizer ameshukuru Jeshi la Polisi kwa kuwajali wazee wanaoishi katika mazingira magumu na kutoa wito kwa makundi mengine kuiga mfano ulioneshwa na Jeshi hilo wa kujali wazee.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...