BENKI ya Exim Tanzania imeendelea kugawa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu na simu janja (smartphones) kwa washindi wa kampeni yake “Chanja Kijanja, Kimasta Zaidi’’ inayolenga kuhamasisha wateja wa benki ya Exim kutumia kadi zao za Mastercard katika manunuzi ya mtandaoni au kufanya malipo kupitia mashine za malipo (POS) katika maduka mbalimbali na maeneo mengine nchini.


Kampeni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi Novemba inatoa fursa kwa wateja wa benki hiyo wanaotumia kadi zao za Exim Mastercard kufanya miamala, kuwa kwenye nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu, Simu janja (Smart Phones) na safari zilizolipiwa gharama zote kwenda mapumziko katika mataifa ya Dubai, Uturuki na Afrika Kusini wao pamoja na wenza wao.
Mkuu wa Idara ya Huduma Mbadala Kupitia Mifumo ya Kidigitali, Benki ya Exim Bw. Silas Matoi (wa pili kulia) akikabidhi zawadi ya simu janja aina ya Iphone 14 Pro kwa Bw. Balubhai Patel (wa pili kushoto) mkazi wa jiji la Dar es Salaam baada ya kuibuka mshindi wa droo ya pili mwezi ya kampeni ya “Chanja Kijanja, Kimasta Zaidi’’ inayolenga kuhamasisha wateja wa benki hiyo kutumia kadi zao za Mastercard katika manunuzi ya mtandaoni au kufanya malipo kupitia mashine za malipo (POS). Wanaoshuhudia ni Meneja wa benki hiyo tawi la Exim Tower Bw. Vishal Ratansinh (kulia) na Afisa Idara ya Huduma Mbadala Kupitia Mifumo ya Kidigitali wa benki hiyo Bw. Gregory Malembeka (Kushoto). Hafla ya makabidhiano kwa washindi hao imefanyika jijini Dar es Salaam leo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...