WIZARA ya Kilimo kwa kushirikiana na kampuni ya JTI Leaf Services watoa mafunzo maalumu kwa wadau wa kilimo cha Tumbaku kuhusu masuala ya kisheria na kisera katika mwenendo wa uzalishaji na uuzaji wa zaohilo Jijini Dodoma hivi karibuni.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Dkt. Batilda Buriani akizungumza wakati wa mafunzo hayo amewapongeza Wizara ya Kilimo na kampuni ya JTI Leaf Services kwa kutoa mafunzo ambayo yataenda kuwasaidia katika utendaji kazi wao.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mh Balozi Dkt. Batilda Buriani akizungumza wakati wa Warsha maalumu iliyoangazia masuala ya Kisheria na Kisera katika mwenendo wa uzalishaji na uuzaji wa zao la tumbaku iliyoandaliwa na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na kampuni ya JTI Leaf Services na kuwahusisha wadau mbalimbali wa tumbaku Jijini Dodoma hivi karibuni. Kulia ni Patricia Mhondo, muwakilishi wa JTI Leaf Services na Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania, Victor Mwambalaswa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...