*TAGCO yampa tuzo Rais Samia

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema Maafisa Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali wanao wajibu wa kuhakikisha wanatoa taarifa za jinsi serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya kipindi cha miaka miwili imefanya. 

Mhe. Majaliwa ameyasema hayo wakati akifungua Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Machi 27, 2023

“Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini, mnao wajibu wa kuhakikisha mnatoa taarifa za jinsi serikali ilivyotatua shida hizo za wananchi kwani kwa kutofanya hivyo wapo watu wengine wataendelea kufanya upotoshaji wakati sisi wanahabari tunajua kuwa huo ni upotoshaji.”” Alifafanua.

Alisema jukumu la kuisemea serikali ni moja ya sehemu ya mawasiliano ya nje ya serikali kwahivyo wanapaswa kuzingatia.

Alisema sambamba na hilo, aliwataka wanahabari wote wa serikali na binafsi wahakikishe wananchi wanapata elimu na  taarifa sahihi kuhusu faida na umuhimu wa miradi na mipango au shughuli zinazotelekezwa na serikali ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa sahihi kwa urahisi  zaidi na kwa wakati.

Aidha aliwataka wazingatie suala la uhuru wa kupata na kutoa habari unaoendelea kutekelezwa kwa mujibu wa sheria, Taratibu na kanuni na wadau wote kila mmoja atimize wajibu wake.

Aliwataka kuimarisha matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuongeza upatikanaji wa habari kwenye maeneo yenu.
“Kila mmoja kutoka mahali alipo, tunazo taasisi za mitandao ya kijamii ambazo zinafanya kazi pamoja na serikali, endeleeni kuwashirikisha katika kutoa taarifa za kazi na shughuli za serikali.” Alisisitiza.

Pia aliwataka kushiriki kikamilifu kuitangaza vema Tanzania ndani na nje ya nchi hususan sula la amani na utulivu, fursa za biashara na uwekezaji, historia ya nchi na kuweka msisitizo katika kufuata maadili na mila za nchi na kutangaza mali kale na vivutio

Aidha aliwataka kuweka mbele uzalendo, uadilifu, uhuru na maslahi ya nchi ili kulijenga taifa na aliwakumbusha kuongeza ubunifu wa kusukuma ajenda za serikali kwa umma.

Hali kadhalika aliwataka kujiendeleza ili kuendana na asi ya mabadiliko ya kiteknlojia.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alisema Kikao hicho ambacho kimewaleta pamoja Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali kutoka Bara na Visiwani  ni muhimu kwa ustawi na mchango wa kada hii katika utekelezaji wa shughuli za kila siku za serikali.

“Kikao hichi kitatumika pamoja na mambo mengine kutathimini mchango wetu katika kusukuma ajenda mbalimbali za serikali na namna ya kuboresha mchango huo.” Alifafanua Mhe. Nnauye.

Katika hatua nyingine TAGCO kimempa tuzo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua na kuthamini mchango wake katika kuimarisha sekta ya habari, demokrasia, uwazi, uhuru wa kutoa maoni na kupata taarifa nchini.

Tuzo hiyo imepokelewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais.

Akikabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya TAGCO, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alisema,  “Sisi maafisa habari serikalini, tumemwelewa, tunamwamini na tunamuunga mkono kwa dhati, Anaishi anayoyasema na anayatenda kwa ustadi mkubwa.” Alisema Mhe. Nape

Kauli mbiu ya Mwaka huu ni "Mawasiliano ya Kimkakati Injini ya Maendeleo".

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (kushoto) akipokea tuzo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye kwa niaba ya TAGCO, wakati wa kikao kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Machi 27, 2023.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, akihutubia kwenye kikao hicho.

Kikao kikiendelea JNICC
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akizungumza kwenye kikao hicho.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye, akizungmza kwenye kikao hicho.
Viongozi wa Kamati ya Utendaji TAGCO.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Selemani Mkomi (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba
Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma NSSF, Bi. Lulu Mengele (kushoto) na Mkuu wa KItengo cha Uhusiano kwa Umma Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Laura Kunenge nao walikuwepo.
Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma (PSSSF) Bw. James Mlowe (kushoto) akiwa na Maafisa Uhusiano wa Mfuko huo, Donald Maeda (katikati) na Coleta Mnyamani.
Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Tanzania Zanzibar
Waziri Nape akipokewa na Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde akiwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Selestine Kakele (wapili kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Mawsiliano cha Wizara hiyo, Bw. Innocent Mungy.
Mhe. Waziri Nape (katikati) akipokewa na Naibu Katibu Mkuu Bw. Selestine Kakele (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa wakati akiwasili. ukumbini.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson wakiagana na viongozi wengine wa serikali.
Katibu Halmashauri Kuu Itikadi na Uenezi wa CCM, Komrade Sophia Mjema (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sara Kibonde.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...