NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
KLABU ya Simba imeweza kufuta uteja mbele ya mahasimu wao Yanga Sc mara baada ya kufanikiwa kuichapa 2-0 kwenye mchezo ambao umepigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Simba Sc ilianza kupata bao la mapema kabisa kupitia kwa Henock Inonga kabla ya Kibu Denis kumaliza mchezo kwa kupachika bao kali na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Yanga Sc sasa itaendelea kuwa kileleni mwa ligi ikiwa na pointi 68 wakiwaacha mahasimu wao kwa pointi tano ambao kwa ushindi wa leo unawapeleka kuwa pointi 63.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...