Na Farida Mangube MOROGORO

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi Mhe. Yose Mlyambina amesema wataendelea kushirikiana na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ili kuhakikisha watumishi wanatekeleza majukumu yao katika hali ya usalama na afya bora.

Ameyasema hayo wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe, Prof. Joyce Ndalichako Aprili 28, 2023 katika Uwanja wa Tumbaku Mkoani Morogoro.

Aidha Dkt Mlyambina Amesema wameandaa mkakati wa kupokea elimu kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Usalama na Afya Mahali pa Kazi ambao utahusisha Menejimenti ya Mahakama, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) na Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi ili kujitathimi na kuzingatia sheria na kanuni za Usalama na Afya mahali pa kazi.

“Katika kuthamini mchango wa OSHA kwa kuheshimu Sheria za Nchi kuhusu umuhimu wa Usalama na Afya mahali pa kazi, mapema mwezi ujao tutatekeleza mkakati huu,” Amesema Dkt. Mlyambina.

Aidha Dkt. Mlyambina amemshukuru Mtendaji Mkuu wa Usalama na Afya mahali pa kazi (OSHA) kwa kuridhia mpango huo wa utoaji Elimu kwa Menejimenti ya Mahakama Kuu Divisheni ya kazi.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi Mhe, Dkt. Yose Mlyambina akitoa hotuba fupi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya mahali pa kazi (OSHA) mbele ya Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe, Prof. Joyce Ndalichako katika viwanja vya Tumbaku Mkoani Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...