KIMANGE

Mkuu wa Mkoa Pwani Mhe. Aboubakar Kunenge ametembeleaeneo la ujenzi wa kalavati lililomomonyoka katika barabara ya Segera-Chalinze eneo la Kimange na kuwataka madereva wa magari kufuata maelekezo ya Askari wa Usalama barabarani mara wafikapo kwenye eneo hilo.

Mvua kubwa iliyonyesha Jumamosi iliyopita, ilimomonyoa kingo ya barabara upana wa mita 60 na kuacha eneo la mita 1;30 ya njia kuwa salama na ambayo ndiyo inatumika.

Mhe. Kunenge amesema mara baada ya hitilafu hiyo, serikali sikifu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia wahandisi wa TANROADS walianza kazi mara moja ya kukarabati eneo hilo kwa kumwaga zege na kuweka makalavati mengine.

“Tumekuwa hapa tangu siku ya kwanza ili kuhakikisha kazi hii inakamilika ili wananchi waendelee na shughuli zao za kujenga uchumi.

“Upande unaotumika ni upande mmoja na hivyo magari yanapita taratibu hivyo kutakuwa na uwingi wa magari niwaombe ukiambiwa subiri wenzako wa upande mmoja wapiti subiri.” Alisema.

Alisema wataalamu wa TANROADS wamemuhakikishia kuwa kazi hiyo inatarajiwa kukamilika leo ingawa itahitajika kiasi cha siku saba ili zege lililowekwa liweze kushikamana vizuri.

Aliwaasa madereva kuwa makini  katika kipindi hiki cha mvua za masika nchini, wanapoona barabara imefunikwa na maji wasijaribu kupita kwani ni hatari.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Aboubakar Kunenge (kushoto) akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Aprili 17, 2023








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...