Njombe
JESHI la Polisi mkoani Njombe imewataka wazazi na walezi katika kipindi hiki cha sikukuu kujihakikishia usalama wa watoto wao pindi wanapoenda katika viunga mbalimbali kwani kwa sasa kumekuwa na unyanyasaji wa kingono kwa watoto na hasa wakiume na kupelekea watoto hao kuharibikiwa maumbile yao.

Kamanda wa Polisi mkoani wa Njombe Hamis Issah amesema watoto watakapotoka matembezini wazazi ama walezi wahakikishe wanawakagua ili kuhakikisha kuwa wapo salama.

"Sasa hivi kumekuwa na mfumuko wa unyanyasaji unaofanywa na watu wazima ama watoto wenyewe kwa wenyewe ambapo hujenga mahusiano ya jinsia moja kitu ambacho ni kinyume cha maadili"amesema Kamanda Issah

Kuhusu tukio la wanafunzi kadhaa katika moja ya shule ya sekondari mjini Njombe kutajwa kusimamishwa masomo kwa kukutwa na makosa mbali mbali ikiwemo mapenzi ya jinsia moja (Ushoga) amesema polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

"Kuna taharuki kwenye mashule ya Sekondari vijana wamejihusisha na mapenzi ya jinsia moja lakini sahizi upelelezi unaendelea itakapokuwa tayari tutaeleza nini kimejiri,na nani amehusika"alisema Kamanda Issah

Aidha amesema jeshi hilo tayari limeimarisha ulinzi katika kipindi hiki cha sikukuu huku akiwataka madereva wa magari mbalimbali kuendesha magari yao kwa uangalifu bila uvunjifu wowote wa sheria ikiwemo kutokutumia kilevi kupilitiza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...