Jeshi la polisi mkoani shinyanga limetoa tahadhari kwa wakazi woto wa mkoa wa shinyanga kuelakea sikukuu za pasaka Aprili 9, 2023 kuhakikisha wazazi wanakua na watoto wao, kutowaruhusu Watoto kwenda kwenye kumbi za starehe, disko na vibanda umiza.
Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari Kamanda wa jeshi la polisi mkoani shinyanga ACP Janeth Magomi amewataka watumiaji wote wa vyombo vya moto kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu zote za barabarani ili kuepuka ajali
Aidha kamanda Magomo amewahakikishia wakazi wote na washerehekeaji wa sikukuu ya pasaka kuwa jeshi hilo limejipanga kikamilifu kuhakikisha washiriki wa sherehe hiyo wanakua salama, huku akiwatakia kheri ya sikukuu ya pasaka wakristo na wanashinyanga kwa ujumla.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...