Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh akizungumza


Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh kulia akiongoza mchezo wa Yoga.
Washiriki wa mchezo wa Yoga wakiendelea nao kwenye Ukumbi wa Hotel ya Mkonge Jijini Tanga

Mchezo wa Yoga ukiendelea

Mchezo wa Yoga ukiendelea
Wageni mbalimbali wakifuatilia mchezo huo

Picha ya pamoja na kikundi cha Yoga cha Jijini Tanga
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga (TPC) Lulu George ambaye ni miongoni mwa wachezaji wa mchezo huo



Na Oscar Assenga,Tanga

BODI ya Mkonge Tanzania (TSB) imeweka bayana kwamba itatumia pia mchezo wa Yoga kuhamasisha Kilimo cha zao la Mkonge ili kuweza kupanua wigo mpana ili kuongeza idadi ya wakulima.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Kambona ambaye alialikwa kwenye shughuli hiyo kama mgeni Alisema mashuhuri kwenye shughuli ya kimataifaa ya Yoga ambapo Tanga wana wanachama wengi ambapo aliweza kujionea shughuli zinazoendelea.

Alisema kwamba baada ya kuona shughuli hizo amejifunza kwamba mchezo wa Yoga ni mchezo muhimu kwa ajili ya afya ya akili na kuweza kuona namna mazoezi yanavyofanyika tumeshuhudia walimu kutoka nchini India wakifundisha kupitia videeo Conference akionyeha mazoezi yanavyokwenda.

Aidha alisema kwamba hivyo wameona ni hatua muhimu kwao kufika na kuna uwekezako wa kutumia mchezo wa Yoga kuhamasisha kilimo cha zao la mkonge kutokana na kwamba wao kila kila fursa wanaiutumia kuona namna ya kuiunganisha na zao la Mkonge.

Alisema kwamba na jambo hilo linafanyika hoteli ya Mkonge ambayo ni Brand kubwa ya zaio la Mkonge Tanga na amefurahi sana na Taasisi ya Yoga ni jambo nzuri sana.

Kwa upande wake Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh aliitaka jamii kutambua umuhimu wa Yoga kwa afya ya mwili,akili na roho na kwamba yatawasaidia katika kuleta mitazamo chanya kwenye mambo mbalimbali ya maisha yao.

"Yoga ni muhimu sana kwenye afya ya mwili ,akili na roho na mtu akifanya hatajutia maamuzi ya kujiunga kwani ataona mabadiliko makubwa kwenye maisha yake," alisisitiza Mratibu huyo wa Yoga kwa Mkoa wa Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...