Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Mkoa wa Singida Martha Mlata ameiomba Serikali kuharakisha kupeleka huduma ya mawasiliano ya mtandao katika Kata ya Makilawa.
Mlata amayasema hayo akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wq Ilani pamoja na kusikiliza kero za wananchi ambapo ametumia nafasi hiyo kutoa ombi kwa serikali kuangalia uwezekano wa kuharakisha kupeleka huduma hiyo ya mtandao wa mawasiliano ya simu kwa wananchi wa kata hiyo
Aidha Mlata ambaye ameambatana na Kamati ya Siasa ya Mkoa , ametumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuebdelea kutekeleza miradi mbalimbali kwa lengo la kuleta maendeleo.
"Naipongeza kwa kazi nzuri ya kusimamia miradi ya maendeleo lakini tunaona iko haja kwa Serikali kuharakisha kuleta huduma mawasiliano ya mtandao ya simu ili wananchi wawe na urahisi katika kufanya mawasiliano."
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...