NA DENIS MLOWE, IRINGA

MKURUGENZI wa Volunteers for Community Development, Justin Nyamoga ametoa msaada wa vifaa vya shule kwa taasisi ya kijamii ya Sauti ya Jamii kwa ajili ya watoto wenye huitaji.

Nyamoga ambaye ni mbunge wa Jimbo la Kilolo mkoani Iringa ametoa msaada huo baada ya kupata maombi kutoka kwa Mkurugenzi wa Sauti ya Jamii kuhusu kampeni ya Mpe Kalamu asome ambayo inahusisha watoto wenye uhitaji.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo Nyamoga alisema kwamba Lengo ni kusaidia jamii katika kuwaondolea changamoto mbalimbali zinazowakabili hivyo msaada huo utakuwa kuwakomboa wanafunzi kwenye masuala ya elimu .

"Taasisi itakuwa na lengo la kujitolea kwenye masuala mbalimbali ya kijamii katika kuleta maendeleo hivyo umuhimu mkubwa ni kujitolea kwa nguvu kazi na Kwa kushirikiana na wadau mbali mbali ndani na nie ya nchi"Alisema

Aliongeza kuwa msaada huo umekuja wakati ambao watoto wengi wanakosa vifaa mbalimbali vya elimu hivyo utakuwa mkombozi hata kama kwa uchache

Nyamoga alikibidhi madaftari , penseli, peni, rula na vifutio kwa taasisi hiyo na kupokolewa na Mkurugenzi wake Jane Mwalwembe ambaye ni mwanaharakati wa kupambana na ukatili wa kijinsia mkoa wa Iringa.

Kwa Upande wake Mwalwembe alishukuru msaada huo kutoka kwa Volunteers for Community Development kuwa umekuja kwa wakati mwafaka na utawafikia watoto wenye uhitaji katika shule mbalimbali mkoani Iringa.

Alisema kuwa Sauti ya Jamii imeanzisha kampeni ya Nipe Kalamu Nisome ikiwa na lengo la kuwapatia mahitaji watoto wenye uhitaji vifaa vya shule.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...