
Mkandarasi huyo amepokelewa na Meneja Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Singida Mhandisi Msama,wawakilishi wa kampuni wakiongozwa na Mhandisi Harold Kitahinda, viongozi wa vijiji vya Makiungu na Mungaa wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Unyanghumpi Mussa Mkanga sambamba na katibu wa Mbunge wa Singida Mashariki Ally Rehani.
Mkataba wa ujenzi wa Barabara hiyo ni miezi 66 na mradi una sehemu nne na zitatekelezwa kwa pamoja.
Wananchi walionyesha shangwe na furaha yao ya kuona mradi huo unaanza baada ya kusubiri kwa muda mrefu.
Katibu wa Mbunge Mtaturu Ally Rehani amewapongeza wakandarasi kwa kuja kuanza kazi kama walivyosaini mkataba tarehe 16 June 2023 pale Jijini Dodoma.
"Mh Mtaturu amefurahi sana kwa jitihada hizi za serikali,na amenituma nifikishe salamu zake kwamba yeye binafsi anatarajia kuona mkizingatia muda wa mradi kwani wananchi wameusubiri kwa muda mrefu ili kuboresha huduma za usafiri," amesema.
Kuanza kwa mradi huo kunakamilisha kazi nzuri iliyofanywa na Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ya kupaza sauti bungeni mara kadhaa wakati akiuliza swali na kuchangia mijadala mbalimbali.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...