WATUMIAJI wa usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro mkoani Geita wameililia serikali juu ya uhaba wa mafuta ya petroli unaoendelea mkoani humo ambapo kwa siku ya leo mafuta yalikuwa yanapatikana katika kituo kimoja tu cha Lake oil kilichopo Nyamigota huku vingine vikiwa vimefungwa .

Wakizungumza na Michuzi Tv bodaboda hao waliwashutumu wamiliki wa vituo vya mafuta kuficha mafuta na kugoma kuyauza huku wakisubiri tamko kutoka kwa serikali la kupandisha mafuta ili wapate faida zaidi.

Kwa Upande wa meneja wa sheli ya Faraja Juma Adam alisema mafuta yamekuwa ya tabu kupatikana hata kwa upande wao pia kwani wanapata mafuta machache kulingana na matumizi ya mjini hapo.

Aidha wananchi hao walisema kuwa ukosefu wa mafuta umekuwa ni kilio kikubwa kwao kwani wengi wao wanaishi kwa kutegemea biashara za kubeba watu kwenye bodaboda yanapoadimika kama hivi inakuwa ngumu sana kwao kuendesha maisha.


Waendesha Pikipiki Maarufu kama Boda boda wa Katoro mkoani Geita wakiwa kwenye foleni kwaajili ya kuweka mafuta ya Petroli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...