Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Godfrey Chongolo akizungumza na wadau mbalimbali wa demokrasia nchini, wakiwemo Viongozi wa Vyama vya Siasa, Waandishi wa Habari, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Asasi za Kiraia na makundi mengine, waliohudhuria uzinduzi rasmi wa Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa na Wadau wa Demokrasia Kutathmini Utekelezaji wa Mapendekezo ya Kikosi Kazi na Hali ya Siasa nchini, uliofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 11, 2023, jijini Dar Es Salaam.

Mkutano huo unaofanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) unawashirikisha Wadau wa Demokrasia, wakiwemo Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Asasi za Kiraia, Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Kimila.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...