Na John Walter-Manyara

Mkuu wa wilaya ya Babati Lazaro Twange ameanzisha mpango wa kusikiliza kero za wananchi kwa kuwafuata kwenye Mitaa na vijiji vyao kupitia ofisi inayotembea (Mobile office) ili waweze kuwafikia kwa wingi zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo septemba 6,2023 amesema kuanzia kesho alhamisi septemba 7,2023 ataambatana na idara, taasisi zote za serikali zilizopo katika wilaya ya Babati kusikiliza na kuzitatua kero zote zilizopo.

Pia, DC Twange amewataka watumishiwote wa serikali kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya sita katika kuwahudumia wananchi.

Amewataka Madiwani, Wenyeviti wa mitaa, vijiji na watendaji wa serikali katika kata vijiji na mitaa kuwahimiza wananchi kufika katika maeneo mkutano utakapofanyika.

Twange amewasihi wananchi kutoa kero, changamoto na matatizo yao bila hofu yoyote kwa kuwa serikali ipo kwa ajili yao.


 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...