Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma Ngollo Malenya anatarajia kuunda tume itakayoshughulikia kuchunguza malalamiko ya wananchi kuhusu uuzaji wa maeneo ya vijiji.
Malenya
amefika uamuzi huo kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji Cha
Songambele baada ya wananchi wa Kijiji hicho kuutuhumu uongozi wa Kijiji
hicho kuhusika na uuzaji wa maeneo ya Kijiji hicho huku uongozi wa
Kijiji hicho kukana kuhusika na uuzaji huo.
Mustafa
Maleka mkazi wa Kijiji Cha Songambele alimwambia mkuu wa wilaya ya
Namtumbo kuwa uongozi wa Kijiji hicho umehusika kuuza maeneo ya Kijiji
bila kufuata utaratibu
Maleka
Adam Maleka Naye mkazi wa Kijiji Cha Songambele alimwambia mkuu wa
wilaya kuwa mwenyekiti wa Kijiji hatoi majibu sahihi kuhusu msitu
uliouzwa na kuharibiwa wa Kijiji hicho.
Mzabuni
Maleka Naye mkazi wa Kijiji Cha Songambele alidai mwenyekiti huyo
alisimamishwa katika nafasi yake kutokana na tuhuma za kushindwa Kutoa
majibu ya uuzaji wa maeneo ya Kijiji hicho , hivyo tunashangaa kumwona
akiwa anaongoza mkutano tena alisema Maleka.
Mwenyekiti
wa Kijiji Cha Songambele Omari Magazini alimwambia mkuu wa wilaya kuwa
tuhuma zinazoelekezwa kwake na uongozi wake hazina ukweli wowote Bali
familia ya Maleka ni familia iliyokuwa inajihusisha na tabia ya ki- Al-
Shabab katika Kijiji hicho.
Magazini
alisema wakati wa operesheni uliofanywa na Serikali kuhusu watu
wanaojihusisha na tabia ya ki_ Al-Shabab Kijiji hicho Cha Songambele
kilitaja familia hiyo kujihusisha na Al Shabab Hali iliyoibua chuki
kwake .
Pamoja
na hayo Mkuu wa wilaya alitoa nafasi Kwa viongozi na wananchi
kuzungumzia tuhuma zinazomkabili mwenyekiti huyo ikaonesha baadhi ya
wananchi kuunga mkono kuuzwa Kwa maeneo ya Kijiji hicho lakini baadhi ya
wananchi kupinga kuuzwa Kwa maeneo hayo Kwa madai kuwa maeneo hayo
yamevamiwa na wafugaji ambao hawana vibali ya kukaa katika maeneo hayo
huku wengine wakidai viongozi wamewauzia.
Kufuatia
sintofahamu hiyo mkuu wa wilaya ya Namtumbo aliwaambia wananchi hao
kuwa ataunda tume ya kuchunguza malalamiko hayo Ili viongozi
wanaokumbatia wafugaji wakibainika kufanya hivyo kutoka kwenye taarifa
ya tume watashughulikiwa .
Mkuu
wa wilaya ya Namtumbo Ngollo Malenya anafanya ziara ya kuzungumza na
wananchi katika vijiji vya wilaya hiyo Kwa kusikiliza kero za wananchi
na Kisha kuzipatia majawabu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...