Na Janeth Raphael MichuziTv - Dodoma

Serikali itaendelea kuboresha mazingira, miundombinu na Huduma kwa Maafisa Ustawi wa Jamii ili wafanye kazi kwa ufanisi.

Akifunga mkutano wa mwaka wa kiutendaji wa Maafisa Ustawi wa Jamii, Septemba 7, 2023 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amesema Maafisa hao wana dhamana kubwa kuhakikisha usalama na amani ndani ya jamii.

"Ajenda hii ni muhimu na imebebwa kwa uzito na viongozi wetu wa kitaifa hususani Mhe. Samia Suluhu Hassan, ndio maana aliunda Wizara hii kwa sababu anajua changamoto, malengo, matatizo ya Watanzania hivyo Maafisa mliopo hapa mtakuwa mabalozi wazuri kwa wananchi, muwapokee, mtatue matatizo yao, wajue kwamba Serikali yao ipo inafanya kazi." amesema Mhe. Mwanaidi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Seif Shekalaghe amesema Maafisa Ustawi wa Jamii ni muhimu sana kwa jamii kwani matatizo mengi yanayotokea hasa ukatili wa kijinsia yanatokana na uwepo wa matatizo ya kisaikolojia hasa Afya ya akili.

"Sisi Makatibu Wakuu na ninyi Maafisa Ustawi wa Jamii ndio watekelezaji wa mambo yote kwa wananchi naamini tukionesha mshikamano nawahakikishia kuwa malengo yetu ya kuwahudumia wananchi yatakuwa yametimia" alisema Dkt. Shekalaghe

Naye Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (Afya) Dkt. Wilson Charles amewaambia Maafisa Ustawi wa Jamii hao kuwa Ofisi hiyo itashirikiana na Mamlaka nyingine kuhakikisha inatatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo uhaba wa Maafisa na vitendea kazi katika kuwahudumia wananchi.

Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii umeshirikisha kutoka Wizara, Mikoa Halmashauri na Taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi ukiwa na kauli mbiu isemayo: Malezi Makuzi na Afya Bora ya Akili ni Jukumu letu sote.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akizungumza na Maafisa Ustawi wa Jamii wakati akifunga Mkutano wa Mwaka wa Maafisa hao uliofanyika Septemba 06-07, 2023 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Seif Shekhalaghe akieleza umuhimu wa Maafisa Ustawi wa Jamii kutumika kwa maendeleo ya jamii wakati wa ufungaji wa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii uliofanyika Septemba 06-07, 2023 jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (Afya) Dkt Wilson Charles akielezea namna Ofisi hiyo unavyoratibu utekelezaji wa Afua mbalimbali za Ustawi wa Jamii katika Mamlaka za Mikoa na Serikali za Mitaa wakati wa ufungaji wa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii uliofanyika  Septemba 06-07, 2023 jijini Dodoma.

Baadhi ya Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa, Halmashauri na Taasisi mbalimbali wakifuatilia shughuli ya kufunga Mkutano wa Mwaka wa Maafisa hao uliofanyika Septemba 06-07, 2023 jijini Dodoma.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...