Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MCHEZO wa fainali ya mashindano ya Ndondo CU umemalizika kwa timu ya soka ya Madenge kuibuka mabingwa baada ya kuichabanga timu ya Kibangu Rangers mabao 2-0 na hivyo kujinyakulia kitita cha Sh.milioni 30.

Fainali ya mashndano hayo imefanyika leo Agosti 3, 2023 katika Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Salaam na kudhuriwa na maelfu ya mashabiki wa soka sambamba na wadau wa michezo nchini.

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi ambaye alikabidhi medali, kikombe pamona na kitita cha Sh.milioni 30 kwa mabingwa huku mshindi wa pili Kibangu Rangers wakikabidhiwa medali na fedha Sh.milioni 20.

Naibu Waziri Mwinjuma pia alikabidhi medali kwa waamuzi wote wa michuano hiyo ya Ndondo Cup huku pia akikabidhi fedha kwa mfungaji bora wa michuano hiyo.

Katika mchezo huo wa fainali ambao ulishuhudiwa na maelfu ya mashabiki wa soka walionekana kufurahia fainali hiyo kutokana na timu zote mbili kutumia kasi, mbinu na akili wakati wa mchezo huo.

Hata hivyo timu ya Madenge walionekana kuwa bora zaidi na hivyo kufanikiwa kushinda mabao 2-0 na hivyo kuwawezesha kuwa mabingwa ikiwa ni mara pili mfululizo.

Mashabiki wa timu ya Kibangu Rangers baada ya kufungwa bao 2-0 wengi wao walikata tama na hivyo kuanza kuondoka wakati mchezo unaendelea huku mashabiki wa Madenge wakiamsha shangwe la ubingwa.


 







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...