KATIBU wa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Ally Juma Rehani amekabidhi kiasi cha Shilingi 150,000 kwa ajili ya matibabu ya mtoto Shedrack Yese anayetakiwa kupelekwa Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa ajili ya matibabu.

Kiasi hicho cha fedha amekikabidhi kwa niaba ya Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ili kumsaidia mtoto huyo anayesumbuliwa na seli mundu (Sickle Cell).

"Mhe Mbunge alipokea maombi yenu ya gharama za matibabu ya mtoto Shedrack, amewapa pole na kunituma niwaletee mchango wake wa matibabu,Mh Mbunge anamuombea matibabu mema apone kwa haraka Insha Allah, "amesema.

Hiyo ni baada ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbwanjiki Omari Kulungu kumpeleka mama wa mgonjwa ofisini kwa mbunge na kuomba msaada wa matibabu ya mtoto huyo.

Wakipokea msaada huo mzazi wa mtoto huyo wamemshukuru sana mbunge kwa moyo wake wa huruma na upendo kusaidia watu wenye uhitaji na kumuomba katibu awafikishie salaam kwa mbunge wao Mtaturu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...