Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (kushoto), akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Hassan Babu (katikati), alipowasili katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambapo anafanya ziara ya siku mbili mkoani humo kusikiliza changamoto mbalimbali wanazopitia wafanyabiashara na kuhamasisha matumizi sahihi ya mashine za Kieletroniki (EFD). Kulia ni Mbunge wa Moshi Mjini, Bw. Priscus Tarimo.

Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Tixon Tuyangine Nzunda (kulia), na Kamishna Msaidizi wa Uchambuzi wa Sera wa Wizara ya Fedha, Bw. William Mhoja (katikati), wakiwa katika kikao cha Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (hayupo pichani) na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Hassan Babu (hayupo pichani), katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mjini Moshi.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro, katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambapo anafanya ziara ya siku mbili mkoani humo kusikiliza changamoto mbalimbali wanazopitia wafanyabiashara na kuhamasisha matumizi sahihi ya mashine za Kieletroniki (EFD).

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (kushoto), akiagana  na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Hassan Babu (kulia), baada ya mazungumzo yao, yaliyofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mjini Moshi, ambapo pia anafanya ziara ya siku mbili mkoani humo kusikiliza changamoto mbalimbali wanazopitia wafanyabiashara na kuhamasisha matumizi sahihi ya mashine za Kieletroniki (EFD).

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Kilimanjaro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...