Na Brown Jonas

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameshiriki katika mbio za Ruangwa Marathon ambazo ziliongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Septemba 9, 2023 Mkoani Lindi.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa Marathon hiyo Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa amesema mbio hizo ni maalumu kwa ajili ya kuchangia vifaa tiba katika vituo vya afya Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi ili kusaidia kuokoa Maisha ya wananchi katika mkoa huo na mikoa Jirani.

Kwa upande wake Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa Wabunge wengine kuandaa mbio kama hizo ili kuibua na kukuza vipaji vya mchezo wa riadha katika maeneo yao hatua itakayosaidia kuwa na timu imara ya taifa ya mchezo huo ambayo itakayokuwa na ushindani ndani na nje ya nchi.

Mbio hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Wadau wa Michezo, Wasanii pamoja na wananchi wa mkoa wa Lindi na mikoa Jirani ambapo mbio zilizoshindaniwa ni KM 5, 10 na 21.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...