WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka wananchi kwenye maeneo mbalimbali nchini washiriki katika michezo kwa kuwa michezo ni ajira, uchumi na huimarisha afya.

Tunapa faida nyingi kwa kufanya michezo, tushiriki katika michezo pamoja na kukimbia riadha kwa kuongeza vipaji tulivyonavyo kwani tukishindana tunapata na zawadi. Michezo ni uchumi.  

Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Jumamosi, Septemba 9, 2023) baada ya kuzindua Ruangwa Marathon katika kiwanja cha Kilimahewa, wilayani Ruangwa Lindi.

Aidha, Waziri Mkuu amesema amemshukuru Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa aliyoyafanya katika sekta ya afya nchini ikiwemo na wilaya ya Ruangwa.

Amesema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika maeneo ya kutolea huduma za afya kwa kujenga zahanati, vituo vya afyfa na hospitali ya wilaya ambayo inavifaa tiba vya kisasa.

Mbio hizo za hisani ambazo zimefanyika kwa mara ya kwanza wilayani Ruangwa zimehudhuriwa na wanariadha mbalimbali wanaoliwakilisha Taifa katika mashindano ya mbio za kimataifa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Molel amesema mbio hizo za marathon ni nzuri kwa sababu mazoezi yanasaidia katika kupambana na magonjwa yasiyoambukiza.

Dkt. Molel amemshukuru Waziri Mkuu kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika mbio hizo za hisani zilizokuwa na lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kununulia vifaa tiba wilayani Ruangwa.

Pia, Dkt. Molel ameishukuru Serikali kwa kuboresha huduma za afya ambapo kwasasa asilimia 97 ya wagonjwa waliokuwa wanapelekwa nje ya nchi kwa matibabu wanatibiwa nchini.

 

(mwisho)

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMAMOSI, SEPTEMBA 9, 2023.

 

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka wananchi kwenye maeneo mbalimbali nchini washiriki katika michezo kwa kuwa michezo ni ajira, uchumi na huimarisha afya.

Tunapa faida nyingi kwa kufanya michezo, tushiriki katika michezo pamoja na kukimbia riadha kwa kuongeza vipaji tulivyonavyo kwani tukishindana tunapata na zawadi. Michezo ni uchumi.  

Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Jumamosi, Septemba 9, 2023) baada ya kuzindua Ruangwa Marathon katika kiwanja cha Kilimahewa, wilayani Ruangwa Lindi.

Aidha, Waziri Mkuu amesema amemshukuru Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa aliyoyafanya katika sekta ya afya nchini ikiwemo na wilaya ya Ruangwa.

Amesema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika maeneo ya kutolea huduma za afya kwa kujenga zahanati, vituo vya afyfa na hospitali ya wilaya ambayo inavifaa tiba vya kisasa.

Mbio hizo za hisani ambazo zimefanyika kwa mara ya kwanza wilayani Ruangwa zimehudhuriwa na wanariadha mbalimbali wanaoliwakilisha Taifa katika mashindano ya mbio za kimataifa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Molel amesema mbio hizo za marathon ni nzuri kwa sababu mazoezi yanasaidia katika kupambana na magonjwa yasiyoambukiza.

Dkt. Molel amemshukuru Waziri Mkuu kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika mbio hizo za hisani zilizokuwa na lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kununulia vifaa tiba wilayani Ruangwa.

Pia, Dkt. Molel ameishukuru Serikali kwa kuboresha huduma za afya ambapo kwasasa asilimia 97 ya wagonjwa waliokuwa wanapelekwa nje ya nchi kwa matibabu wanatibiwa nchini.

 

Waziri Mkuu na Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary Majaliwa (kushoto kwake) wakishiriki katika mbio za Ruangwa Marathon kwa ajili ya kuchangia vifaa tiba zilizofanyika Ruangwa, Septemba 9, 2023. Kulia kwake ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro na kushoto ni Mkurugenzi wa Wasafi Media, Nasib Abdul maarufu Diamond Platnum. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akizungumza katika mbio za Ruangwa Marathon zilizofanyika mjini Ruangwa, Septemba 9, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...