Na Nasra Ismail, Geita

Watumishi wa serikali wameonywa kutokufanya udanganyifu ili kupata uhamisho kutoka katika vituo vyao vya mwanzo ili kupunguza uhaba wa watumishi katika maeneo husika.

Akizungumza na watumishi wa serikali katika halmashauri ya mji wa Geita Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala bora George Simbachawene alisema kuwa waliofanya udanganyifu tayari wameshajulikana na wanasubiri kuchukuliwa hatua.

Simbachawene aliongeza kuwa watumishi wengi wana uhamisho ambao ni wa uongo na utapeli na pia wameupata kwa kutoa rushwa.

Aidha Simbachawene aliwaasa watumishi ambao wamefanya udanganyifu ili kupata uhamisho warudi walikotoka kwani wasipofanya hivyo watafukuzwa kazi.

“tukigundua tutawarejesha walikotoka, na kwa maneno haya nayosema yule ambaye alihama kwa uhamisho wa uongo uongo na ameshindwa kuhamisha mshahara wake navoongea hapa arudi alikotoka vinginevyo atafukuzwa kazi” alisema Simbachawene.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...