Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah (kushoto) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia kulinda hakimiliki za Ubunifu duniani -WIPO Bw. Daren Tang ( Kulia) makao makuu ya Shirika hilo Mjini Geneva, Uswisi, tarehe 13 Septemba,2023. 

Mazungumzo yao yalilenga kuimarisha ulinzi wa haki miliki za ubunifu na ushirikiano wa kimataifa ambapo Dkt. Abdallah amemshukuru Bw. Tang kwa ushirikiano Mkubwa ambao WIPO imekuwa ikiutoa, ikiwemo ushauri wa kitaalamu kuhusu uanzishwaji wa Sera ya Taifa ya haki miliki na ubunifu Tanzania bara, kuanzishwa kwa sera ya haki miliki na ubunifu Zanzibar na kuanzishwa kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji nchini Tanzania. 

Bw. Tang ameipongeza Tanzania kwa mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mradi wa hakimiliki nchini.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...