Na. WAF - Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe amesisitiza umuhimu wa kuweka mfumo wa muunganiko kati ya Wizara ya Afya na TAMISEMI ili kuwa na muunganiko mzuri wa kujua idadi ya watumishi pamoja vifaa tiba.

Dkt. Magembe ameyasema hayo Septemba 7,2023 wakati wa mkutano wa kitengo cha huduma za uchunguzi wa magonjwa ukiendelea pamoja na wadau wa huduma za uchunguzi wa magonjwa uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

“Wizara ya Afya pamoja na TAMISEMI kwakweli tunahitaji kuweka mfumo mzuri wa muunganiko kati ya Wizara ya Afya na TAMISEMI ili kuwa na muunganiko mzuri wa kujua idadi ya watumishi pamoja vifaa tiba”. Amesema Dkt. Magembe

Aidha, Dkt Magembe amewaomba wadau hao kuendelea kusaidia kuimarisha mifumo yetu inayoweza kutambua baina ya wizara ya afya na TAMISEMI ili fedha zinazopatikana ziweze kutumika kwa ufanisi na kutatua changamoto za uchunguzi wa Afya kwa wananchi.

“Kwakweli wadau wetu tunawaomba muendelee kusaidia katika kuimarisha mifumo hii ili tuweze kujua na kuona fedha zinapopatikana lakini pia tujue namna zinavyotumika katika kutatua changamoto za wananchi”. Amesema Dkt. Magembe

Vilevile Dkt. Magembe amesema uchunguzi wa kisayansi ni taaluma inayohitaji ushirikiano wa karibu hivyo wadau wa huduma za uchunguzi wa magonjwa na kitengo cha huduma za uchunguzi wa magonjwa wanapaswa kukaa pamoja ili kuelewa nani anahitaji msaada na jinsi ya kushirikiana katika kutumia data nyingi zinazozaliswa.

Pia, amesema kuwa ni muhimu sana kuimarisha huduma za uchunguzi, haswa kuanzia ngazi ya Msingi, tunawaomba wadau wote kuwa na mtazamo wa Kisekta na kuwa wataalam ili iwezekane kuoatikana kwa majibu sahihi na kuepuka kuwachanganya wananchi.

“Tunaona kuna umuhimu mkubwa kwa wadau wetu kuanza na mtazamo wa Kisekta kuanzia ngazi ya msingi kwakuwa wananchi ndipo wanapoanzia kupata huduma hadi ngazi ya juu kwa kuimarisha huduma za uchunguzi”. Amesema Dkt. Magembe
Mwisho, Dkt. Magembe amesema Idara ya huduma za uchunguzi wa magonjwa inapaswa kutoa mwongozo katika kuhakikisha kuwa sekta zote zinashirikiana kwa ufanisi kwenye utafiti hadi utekelezaji.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...