Na. WAF, Mtwara.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka watumishi wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini kuhakikisha kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa na Rais Samia Suluh Hassan katika Hospitali hiyo ikiwemo ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa, kuajiri watumishi pamoja na uhakika wa upatikanaji wa dawa unaendana na ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Waziri Ummy ametoa wito huo leo Septemba 15,2023 wakati akizungumza na Watumishi wa Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua Hospitali hiyo

Aidha Mhe. Ummy amewapongeza watumishi kwa huduma bora zinazotolewa huku akiwasitiza kufanya kazi kwa kuzingatia weledi, maadili na viapo vya Taaluma zao.

“Niwapongeze sana kwa huduma bora mnazozitoa, hospitali hii ina jengo zuri sana, vifaa tiba kwaiyo kilichobaki ni ubora wa huduma”. Ameeleza Waziri Ummy

Mhe. Ummy Mwalimu amewahakikishia watumishi wa hospitali hiyo kuwapatia gari aina ya Coaster moja kwa ajili ya kuwarahisishia kufika kazini.

“Tutaleta angalau gari moja ili kuwarahisishia watumishi kufika kwa wakati eneo la kutolea huduma” , amesisitiza Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa ataendelea kuwa balozi wao kwa kuwasema, kuwalinda, pamoja na kuwatekelezea stahiki zao lakini kila mtumishi atimize wajibu wake ili kuleta ubora wa Huduma kwa wananchi wanao wahudumia.










 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...