Raisa Said ,Tanga
Mkoa wa Tanga Umezindua rasmi Mpango Jumuishi wa Taifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto (PJT_MMMAM) ambapo Wazazi wametakiwa kuuunga mkono mpango huo ili kuboresha kiwango kisichorishidhisha cha watoto wenye umri kati ya miaka 0 hadi 8 ambao hawajafikia ukuaji timilifu.
Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Kanali Maulid Hassan Sarumbu, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba alizindua mpango huo kwa melekezo kwa maafisa wa serikali, viongozi na taasisi kuhakikishat uekelezaji wake unafanyika kwa ufanisi.
“Ili kufikia matarajio ya watoto wa Kitanzania, wazazi na sekta binafsi wawekeze katika maendeleo ya watoto wadogo kuanzia mwaka 0 hadi miaka name" Alisema
Kwa mujibu wa Joel Mwakapala, mwakilishi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii (Programu Maalum), programu hii, iliyozinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan mwaka 2021, ina malengo ya kuwapa watoto wenye umri kati ya miaka 0 na 8 uwezo kufikia ukuaji timilfu.
Alisisitiza umuhimu wa ahadi hii, akihakikisha kwamba kila mtoto anaongozwa kuelekea wakati ujao mzuri, na kukuza kimamaendeleo.
Mwakapala alisisitiza kuwa Rais anatambua umuhimu wa watoto kama rasilimali muhimu ya taifa. Rais alisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika malezi ya awali na maendeleo ya watoto, akisema kuwa sio faida tu ya watoto wenyewe bali pia ni kwa taifa zima.
Alisema mpango huo kwa sasa unazinduliwa katika mikoa 16, ikiwamo Tanga. Mikoa 10 ilikwisha zindua mpango huo.
Kwa mujibu wa Dk. Regis Temba, Mkurugenzi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya UHTC alieleza kuwa asilimia ya watoto wenye umri kati ya miaka
sifuri hadi miaka 8 katika mkoa wa Tanga ambao wamefikia ukuaji timilifu ni 46.
Wakati wa mahojiano baada ya Mpango kuzinduliwa rasmi, Dk. Temba alisisitiza kuwa asilimia 53 ya watoto katika mkoa huo bado Hawajafikia utimilifu wa ukuaji.
Alisisitiza kuwa hatua ya utotoni ina ushawishi mkubwa sana katika maisha ya mtoto. Alidokeza kwamba ikiwa kuna upungufu wowote katika
maendeleo yao wakati huu muhimu, inaweza kuwa na matokeo ya muda mrefu ambayo hatimaye huzuia nafasi zao za kufikia uwezo wao kamili katika maisha ya baadaye Alisema mpango huo unalenga kuimarisha na kuinua kiwango cha maendeleo na makuzi ya watoto wachanga katika mkoa huo.
.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...