Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba Bw. Silvest Arumasi, amezindua rasmi wiki ya huduma kwa wateja katika tawi la Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Arumasi amewashukuru wateja kwa kuichagua na kuiamini Benki ya Akiba katika kuwahudumia. Aidha, ameendelea kuwaahidi na kuwahakikishia wateja huduma bora kutoka ACB.

Sherehe za huduma kwa wateja zina adhimishwa katika matawi yote ya ACB na hivyo, Bw. Arumasi amewaalika wateja wote kutembelea matawi ya Akiba kwa ajili ya kusherekea wiki hii ya huduma kwa wateja pamoja na kupata taarifa mbali mbali za huduma mpya na maboresho mbali mbali.

Pia, Mkurugenzi amewashukuru wateja wote walioshiriki katika zoezi la utafiti wa viwango vya uridhikaji katika utoa huduma yaani (Customer Satisfaction Survey) lililoratibiwa na kampuni huru ya kujitegemea kwa lengo la kuhakikisha uwazi na uhuru wa kutoa maoni kwa wateja.

ACB ina utamaduni wa kufanya utafiti huo kila mwaka na hivyo amewasihi wateja kushiriki tena kikamilifu kwa lengo la kupata maoni na mirejesho itakayosaidioa kuboresha huduma zitolewazo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...