Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 3 Oktoba, 2023 amewasili Accra nchini Ghana na kupokelewa na mwenyeji wake Spika wa Bunge la nchi hiyo Mhe. Alban Bagbin.

Dkt. Tulia anatarajia kushiriki Mkutano wa 66 wa Kibunge wa Jumuiya ya Madola (CPC) utaofanyika nchini humo kuanzia tarehe 3-6 Oktoba, 2023 yenye dhima isemayo “Miaka 10 ya Mkataba wa Jumuiya ya Madola: Maadili na Kanuni za kuzingatiwa na Mabunge”

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akisalimiana na kuzungumza na Spika wa Bunge la Ghana Mhe. Alban Bagbin wakati alipowasili katika Jiji la Accra, Ghana ambapo anatarajia kushiriki Mkutano wa 66 wa Kibunge wa Jumuiya ya Madola (CPC) utaofanyika nchini humo kuanzia tarehe 3-6 Oktoba, 2023.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...