NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV
Katika kuadhimisha Siku ya Viwango Duniani, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wadau na wananchi kushiriki vyema katika uandaaji wa viwango ili kwa pamoja tuweze kuandaa viwango vinavyotekelezeka .
Akizungumza na Waandishi wa habari leo Oktoba 13,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Viwango Bw.Yona Afrika amesema kuna umuhimu mkubwa wa wadau kushiriki katika uandaaji wa viwango kwani viwango vinasaidia uzalishaji wa bidhaa bora nchini na kuweza masoko makubwa ndani na nje ya nchi.
Aidha amesema kuwa viwango vinasaidia kupunguza gharama pamoja na kukuongezea wateja kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.
Amesema suala la uandaaji wa viwango linahusisha wadau wote wa uzalishaji wa bidhaa na sio la Shirika la Viwango pekee.
Siku ya Viwango Duniani huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 14 kila mwaka


Akizungumza na Waandishi wa habari leo Oktoba 13,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Viwango Bw.Yona Afrika amesema kuna umuhimu mkubwa wa wadau kushiriki katika uandaaji wa viwango kwani viwango vinasaidia uzalishaji wa bidhaa bora nchini na kuweza masoko makubwa ndani na nje ya nchi.
Aidha amesema kuwa viwango vinasaidia kupunguza gharama pamoja na kukuongezea wateja kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.
Amesema suala la uandaaji wa viwango linahusisha wadau wote wa uzalishaji wa bidhaa na sio la Shirika la Viwango pekee.
Siku ya Viwango Duniani huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 14 kila mwaka


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...