Na Mwandishi wetu, Mirerani

BARABARA ya kutoka mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara hadi lango kuu la ukuta unaoingia na kutoka kwenye migodi ya madini ya Tanzanite kuanza kujengwa.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita moja itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, hivi sasa kwa kugharimu kiasi cha fedha cha shilingi bilioni moja.

Meneja wa TARURA Wilayani Simanjiro, mhandisi Naftal Chaula akizungumza kwenye ziara ya Waziri wa Madini Anthony Peter Mavunde amesema barabara hiyo imeshapata mkandarasi wa ujenzi.

Mhandisi Chaula amesema hatua waliyofikia ni mkataba kusainiwa wanafanya kazi ya kusanifu ili ujenzi wa barabara hiyo uanze mara moja kwa mwaka huu wa fedha.

Amesema wameshachukua udongo na kuupeleka maabara ya TANROAD mkoani Kilimanjiro na ukishapimwa na kutolewa majibu wataanza kufanya kazi ya ujenzi wa barabara hiyo.

“Pia tumezungumza na wenzetu wa TANROAD mkoani Manyara, ili tushirikiane nao, kwani hali ya maji ni mbaya kwa hapa hivyo waongeze karavati lingine kudhhibiti hali hiyo,” amesema mhandisi Chaula.

Amesema mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo ya lami unaonyesha kuwa ulipaswa kuanza mwezi Septemba mwaka 2023 na kumalizika Februari mwaka 2024.

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Queen Cathbert Sendiga amesema fedha za ujenzi wa barabara hiyo shilingi bilioni moja ni kati ya shilingi bilioni 6 zilizotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa barabara za wilaya hiyo.

Sendiga amesema fedha hizo ni matengenezo ya barabara za changarawe, makalavati na madaraja hivyo ni matarajio ya Serikali changamoto ya miundombinu hiyo itatatuliwa.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...