Na Mwandishi wetu, Simanjiro

MBUNGE wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka, amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa namna alivyowapatia fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ole Sendeka ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye ziara ya siku moja ya Waziri wa Madini, Anthony Peter Mavunde, alipotembelea mji mdogo wa Mirerani.
 
Amesema katika kipindi kifupi cha utawala wa Rais Dkt Samia, miradi mingi imetekelezwa wilayani Simanjiro, hivyo hawana kitu cha kumlipa zaidi ya asante na kumpa kura nyingi za ndiyo mwaka 2025.

“Rais Dk Samia ametufanikisha kwa fedha zake miradi ya maji, zahanati mpya 11 hapa Simanjiro, miradi ya barabara ya lami ikiwemo ya kutoka Arusha inayopita Simanjiro, Kiteto hadi Kongwa mkoani Dodoma,” amesema Ole Sendeka.

Amesema hata barabara ya lami ya kilomita moja, kutoka mji mdogo wa Mirerani, hadi lango la kuingia kwenye machimbo ya madini ya Tanzanite, imeanza kujengwa ambayo imekaguliwa na Waziri Mavunde.    

“Pamoja na hayo tunampongeza Waziri Mavunde ambaye amekuja na kauli mbiu yake ya Vision 2030 madini ni maisha na utajiri, hivyo tumpe ushirikiano wa kutosha kwenye sekta ya madini,” amesema Ole Sendeka.

Kwa upande wake, Waziri Mavunde amempongeza Ole Sendeka, kwa namna anavyofanya kazi yake ya kuwasemea wananchi wa jimbo la Simanjiro, akiwa Bungeni.

Waziri Mavunde amewasihi wakazi wa Simanjiro kumpa ushirikiano mbunge huyo Ole Sendeka, kwani ni mzoefu na mwenye upendo wa kuwatetea wananchi wake. 



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...