Na Brown Jonas - WUSM
Waziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na
kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Binaya
Pradhan ambapo pamoja na mambo mengine viongozi hao wamejadili kuhusu
tukio la mbio za pamoja za kudumisha ushirikiano kati ya Tanzania na
India "The Friendship Run between India and Tanzania with Milind Soman"
linalotarajia kufanyika jijini Dar es salaam kati ya tarehe 30 na 31
Desemba,2023.
Akizungumza kuhusu tukio hilo leo Desemba 5,2023
Mhe. Ndumbaro amesema Serikali ya India imeomba ushirikiano na Serikali
ya Tanzania kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ili
kufanikisha tukio hilo ambalo pia litahudhuriwa na mwanariadha maarufu
kutoka nchini India Milind Soman.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...